You are most welcome to visit my site. I hope here you will  find the information that you are searching for. Please  be tolerant and patient with me, as this is a bilingual site (English/Swahili). Sometimes you might encounter an article written both in English and Swahili but most of the times it will be in  one language only.

The site mostly covers debates, in the written form,  that took place in different discussion forums, which I had  with my  colleagues. For this reason you will not only find my very own Swahili-English articles but those of  my colleagues as well. 

________________________________

Madhumuni ya kuunda hii site ni kutokana na ile site ya mawaidha ambayo imeweka kwa makusudi ya kuwadhalilisha Mashiya, kuwakufurisha Mashiya na kueneza chuki na fitna za Kimadhehebu. Kwa upande wangu, ikanibidi nichukuwe khatwa ya kujibu tuhma zilizowekwa na muandalizi wa site ya Mawaidha.

Nitamuomba kwa yule atakaepitiya site yetu, isije kumpitikiya kuwa kusudio la kuiweka site hiyo ni kutaka ugomvi baina yetu na Sheikh wa Site ya Mawaidha, kwasababu hiyo sio nia yetu. Tunachokifanya sisi, ni kujibu zile hoja za Kiwahabbi alizoziweka Sheikh wa Mawaidha, kwasababu tumeona kuwa ipo haja ya kujibiwa kwa kila tuhma alioiweka.

Tutaona yakuwa lengo na tegemeo la mwandishi wa hiyo site ya mawaidha ni kutaka kumwaga mbegu za chuki kwa Wazanzibari kwa kuwafanya Mashiya sio Madhehebu sahih na kuwatoa katika Uislamu. Jambo hilo siyo geni khasa tukiwasoma wenye itikadi potofu kama akina Ibn Taymiya wenye fikra kama hizo. Tukiangaliya vizuri tutaona yakuwa muandishi wa hiyo site ni mmoja wa wafuasi wa Ibn Taymiya ambae kwa sasa wenye kujulikana kwa jina la Mawahabi!

Tutamuona yakuwa muandishi wa hiyo site ya mawaidha amejikaza kutaka kupanda hiyo mbegu ya chuki kwa kutumiya vitabu vya Kishia. Cha kustaajabisha kwa upungufu wake wa elimu hakuweza kutambuwa yakuwa itikadi za Mashiya siyo kama za kwake, Mashiya hawana hiyo imani yakuwa vitabu vyao vya hadith ni SAHIH, kama tunavyoona Sahih Bukhari na vyenginevyo. Tumeweza kuthibitisha mara kwa mara wakati tulipokuwa tukijadiliana nae kwa kumuona vipi alivyokuwa akihangaika na kutapatapa kwa kuziteteya hizo hadithi ambazo kwa yoyote yule mwenye kuzisoma kwa uangalifu ataona hadithi zilizomo ndani ya vitabu vinavyojulikana vitabu vya sahih, haziwezi kuwa ni sahih zote kama vile Sheikh wa Zanzinet anvyoziweka yeye. Tunatarajia siku za mbele kudondowa baadhi ya hadithi ziliyomo ndani ya vitabu vinavyoitwa Sahih kwa kuonesha hadithi ambazo haziwezi kuingiya akilini hata kidogo.

Kwa Mashiya, hawana haja ya kuhangaika na kusumbuka jawabu yao safi kama hadith haingi akilini basi hutupiliwa mbali. Huu ndio msimamo wa Mashiya.

 

                                          

 

Hit Counter