Date: Sun, 03 Oct 99 13:33PM MDT

From: "Mohammed Y.Jaffer" <abulqassim@usa.net>    

To:  zanzinet <zanzinet@zanzinet.org>

Cc: abulqassim@usa.net

Subject: [zanzinet] Re: [Re: Utukufu Wa Mtume Muhammad (s.a.w)]

 

HADITH ZA UPUZI

Maneno ya Mohammed Faraj

"Ama kuhusu uwezo wa Mitume (AS) kuwaingilia wanawake zaidi ya 30, sijui

maneno hayo yametokea wapi, lakini mimi sikuyasema maneno hayo. Lakini

ukitaka nizungumzie juu ya uwezo wa Mitume (AS) kufanya hayo basi nitanukuu

kutoka katika vitabu vyenu vitukufu vya Kishia vilivyoandikwa na Maulamaa

wenu;

Katika kitabu kiitwcho AL Burhan 4/49 na kitabu cha Furu-u l Kafi 5/567

imeandikwa hivi;

"Kutoka kwa Hasan bin Jaham anasema; ' Abil Hasan alinambia;

"Suleiman bin Daud alikuwa na wake elfu moja ndani ya kasri yake ......

(mpaka mwisho wa hadithi akasema) "ALikuwa akiwaingilia kila usiku"

Na imenukuliwa kutoka kwa Neemat AL Jazairi(naye pia ni Mshia) kutoka

katika

kitabu cha "QIsasul Anbiyaa" ukurasa wa 407, na hiki ni kitabu cha Mashia .

Imenukuliwa kuwa;"

 

Maneno yangu

Mimi sikusema yakuwa hayo maneno amesema yeye, nimeleta kwa kutaka kuongeza nguvu hoja yangu.

Hizo vitabu alizozitaja sisi hatuzitambu kuwa ni VITABU SAHIH, SASA MIMI NIMESHAYAKATAA

HIZO HADITH YAKUWA DHAIFU, BASI MWACHE NA YEYE AFANYE KAMA NINAVOFANYA

MIMI. Haina haja ya kwenda juu chini kutaka KUITETEA HADITH ZA UPUZI NA ZA UWONGO KUHUSU

MTUME WETU (S.A.W) AU MITUME WENGINE. BADILI YA KUMTETEA MTUME WETU (S.A.W)

NAONA NDUGU AMECHAGUWA KUTETEA HIZO HADITH, MAMBO YA KUSTAAJABISHA!

 

SIFA ZA ALI (A.S)

Maneno ya Mohammed Faraj

Sifa za ALi bin Abi Talib(RA) Kuhusu sifa zenu mnazompa Sayiduna Ali Bin Abi Talib(RA) zisizoweza kukubalika

 na yeyote mwenye akili timamu , hilo ni shauri lenu. Na haya  hamjaanza nyinyi, maana kabla yenu alikuwepo

Myahudi mmoja aitwae Abdillahi bin Saba-a aliyeingia katika dini hii kwa nia ya kutaka kuifisidi. Huyu ni katika

 Mashia wa mwanzo wa ALi(RA), na mtu huyu alipindukia mpaka katika kumsifia ALi(RA) hata akafikia

 kumwambia ALi kuwa yeye ni Allah, na Ali(RA)akamhukumu kuuyliwa kwa kumchoma moto kwa ajili ya kufru

yake hiyo. Soma kitabu cha AL Hilmy ukurasa wa 164 juzu ya 2 (hiki pia ni kitabu cha Kishia).

 

 

Maneno yangu

Hapa ndugu ameleta mada mbili pamoja, ya mwanzo kuhusu hadith zinazomhusu Imam

Ali (a.s) na yapili kuhusu Abdullah ibn Saba.

 

HADITHI KUMHUSU IMAM ALI (A.S)

Bado ndugu anaendelea kunistaajabisha. Ikiwa ninapoletea hadith kuhusu Imam

Ali (a.s) zaidi ninatowa kwenye vitabu vyenu ambae hadith ngapi zingine ni

Mutawwatir na kukubaliwa na Maulama wa Kisunni.

 

ABDULLAH BIN SABA

Mwenye kuleta hadith kuhusu Abdullah bin Saba ni Sayf Ibn Umar al-Dhabbi

al-Usayyidi al-Tamimi, ambae amefariki katika 170 AH, katika wakati wa Haroon

al-Rashid. Sayf ameandika vitabu viwili ambae ilikuwa inapatikana wakati wa

hukum ya Bani Ummaya. Vitabu vyenyewe ni "al-Fotooh wa al-Riddah" inaelezea

tarikh kutoka kabla kufariki Mtume (s.a.w) mpaka wakati wa Khalifa wa tatu. Na

kitabu cha pili ni "al-Jamal wa Maseeri Aisha wa Ali" inaelezea tarikh kutoka

uwaji wa Uthman mpaka vita ya Jamal.

 

Huyu jamaa Sayf anajulikana kuwa ni MUONGO NA MWENYE KUTUNGA HADITH ZA UWONGO,

KAMA HADITH ZA ELFU LAILA WA LAILA. Maualam maaruf wa Kisunni wamethibitisha yakuwa

huyu Sayf ibn Umar alikuwa Maarufu mwenye kujulikana kwa Kusema UWONGO, kama al-Hakim,

 al-Nisa'I, Yahya Ibn Mueen, Abu Hatam, Ibn Abi Hatam, Abu Dawud, Ibn Habban, Ibn Abd al-Barr,

al-Darqutini, Firoozabad, Ibn al-Sakan, Safi al-Din, Ibn Udei, al-Suyuti and Ibn Hajar al-Asqalani.

 

Hata hiyo kitabu ya Kishia iliyoandika kuhusu huyu Abdullah bin Saba haipo katika vitabu nne maaruf.

Kitabu al-Kushshi ameleta hadith nyingi dhaifu na isiyokubalika. Tuseme yakuwa kweli huyu mtu

alikuwepo na ameunguzwa na Imam Ali (a.s), sasa itakuwa ndio nini? Maulama wa Kishia wanamehaesabu

huyu Abdullah ibn Saba ni Munafiq. Ikiwa mtu Munafqi ametokeza kuwa rafiki wa Ali

(a.s) atakuwa anayo kitu gani yakumfanya yeye awe Shia? Ikiwa Mwizi amepanda

kwenye Mimbar na ameleta athari mbaya na kuharibu jina la Islam, je na sisi

tuwachukiye hao Maulama na tuwaite ni Wezi?

 

Ukisoma hiyo hadith ya Elfu laila wa laila ya huyu Sayf utaona hata Masahaba

wakubwa ambae walikuwa wakijulikana kuwa Shiatu Ali kama Abu Dhar na Ammar

Yasir walikuwa wanafunzi wa huyu Abdullah ibn Saba. Jee inaingia akilini watu

hao wamuache Ali (a.s) na kuenda kumfuata huyu Myahudi, na hali wao ndio wenye

kusikia hadith za Mtume (s.a.w) kuhusu Ali (a.s)?

 

Naona ndugu yetu atatafuta kila chochote mbaya apate kuwapachika hao Mashiya hata ikiwa ya Uwongo

na kuwacha ya Ukweli. Nitapenda ndugu yetu awache kuleta hizo hadith za UWONGO NA KULETA HADITH

 ZA UKWELI, KWA MFANO YA KAAB AL-AHBAR. Nitapenda atueleze huyu RABBI YAKIYAHUDI

ALIYEKUWA KARIBU NA KHALIFA WA PILI NA WATATU, NA VIPI WAO WAKICHUKUWA

SHAURI YAKE. SIO KUTULETEA HADITH ZA ELFU LAILA WA LAILA YA SAYF AL-KAZAB!!!!!

 

Wassalam

 

Mohammed Yusuf

 

 

Date:  Tue, 05 Oct 99 05:31AM MDT

From:  "Muhammad Aly" <muhammadaly@hotmail.com>    

To:  abulqassim@usa.net

Cc: zanzinet@zanzinet.org

Subject: Re: Utukufu Wa Mtume Muhammad (s.a.w)(nyongeza)

 

 

Bismillah

Assalam Alaykum

 

Wananeti wote, ………………

 

 

Huko kutaja kwako kwa Abdullah Bin Sabaa kunastaajabisha, wewe ni mtu wa Elimu, mambo mengine hayafai

 kuambiwa, habari za Abdullah Bin Sabaa Sheikh Mohammed Faraj zimepitiwa na wakati na umeshaelezwa humu

 lakini kwa kukuongezea tu, mtu huyu hakupata kuishi Duniani, na habari zake zote ni uzushi wa huyo

Saif Bin Omar At-Tamimi, ukitaka kujuwa zaidi ya ukweli wa maneno haya, Maulamaa wa Kiislamu wengi

waliotabahari kwenye Ellimu za Tariikh wanaona kuwa mtu huyu hakluwepo bali hiyo ilikuwa ni silaha moja wapo

 ya kutaka ama kunusuru heshima ya masahaba ama silaha dhidi ya nguvu ya Ushia uliowapa tabu kisiasa na

kijamii watawala wa kibanu Umayyah na wengineo...Hivyo kwa ajili hii Maulamaa wa Kisunni na wa Kishia wamekataa

kuwepo kwa mtu huyu kwa hoja madhubuti zilizochukuliwa kwenye Vitabu vyote unavyovijuwa na usivyovijuwa

 vya Tariikh ya Kiislamu...Tazama ushahidi wa haya kwenye:

(i) Kitabu "Abdullah Bin Sabaa, cha Allamah Seyyid Mortadha Al-Askari. na kwa wanavyuoni wa Kisunni soma

(ii)Kitabu "Adullah Ibn Sabaa: A Study Of the Historical Resources Concerning His Role in Al-Fitnah" cha

Sheikh Abdul-Aziiz S. Al-Helaabi, Dean wa Kitivo cha Tariikh kwenye King saud University- Saud Arabia..

(iii)Kitabu " Adh'waa ala Sunnati Muhammadiyyah" cha Sheikh wa Azhar miaka ya 1950s Mahmoud Abu-Rayyah

 na kadhalika..

Tanbihi: Dalili zilizomo kwenye Vitabu hivi zitakutosha na huhitaji hoja nyengine zo zote na baada ya kusoma

Vitabu hivi nakuomba utuletee maoni yako juu ya habari za huyu Abdullah Bin Sabaa mnayedai kwa kutegemea

 Hadithi za waongo akina (Saif Bin Omar tamimi) ambaye mimi namwita "Bunuwasi" wa hadithi kama Wanavyuoni

 wote wa Kishia na Kisunni wanavyomwita, umeona listi ya wanavyuoni wa Kisunni walivyomkataa

Seif Bin Omar tamimi  kwenye makala ya bwana Mohammed Yussuf Jaffer, tunaomba wananeti watafakari kwenye

mambo ya hakika na wayatupilie mbali mambo yaliyopitiwa na wakati...

 

Ahsanteni,

Samahani kama nimetumia lugha mbaya, naomba samahani kwa wananeti wote....Ndugu yenu, Muhammad Aly.